Monday, January 19, 2015

TAARIFA KWA UMMA KUTOKA MAMLAKA YA HALI YA HEWA NCHINI:: MVUA KUBWA INATEGEMEWA KUNYESHA MIKOA YA PWANI, RUVUMA NA MOROGORO


Leo Mamlaka ya hali ya hewa Imetoa taarifa kwa Umma kuwa Kuanzia Januari 18, 2015 Mpaka Januari 20, 2015 Kunategemewa kutokea Mvua Kubwa inayozidi milimita 50 ndani ya saa 24, Maeneo ambayo yanatarajiwa kuhusika ni Maeneo ya Mikoa ya Ruvuma, Mtwara, Lindi, Morogoro, Pwani, Dar es Salam na Kisiwa cha Unguja.

Sababu za Mvua hiyo ni Kuimarika kwa Mgandamizo mdogo wa Hewa katika Eneo la Bahari ya Hindi mashariki mwa kisiwa cha Madagasca na Hivyo kusababisha ongezeko la unyevunyevu kutoka misitu ya Kongo kuelekea maeneo tajwa hapo juu.

Mamlaka Imetoa angalizo kuwa wakazi wa maeneo yaliyotajwa hapo juu na Mamlaka zinazohusika na Maafa wanashauriwa Kuchukua hatua stahiki.

Pia imesisitiza Inaendelea Kufuatilia hali hiyo na itatoa mrejesho pale itakapobidi.

No comments:

Speak Your Mind

Powered By Blogger · Designed By Seo Blogger Templates