Hatimaye kiungo Jonas Mkude amesaini mkataba wa miaka miwili kuichezea Simba.
Mkude ambaye ni tegemeo katika kiungo cha ulinzi cha Simba, amesaini mkataba huo leo mbele ya Rais wa Simba, Evans Aveva.
Pamoja na Aveva na viongozi wengine wa Simba akiwemo Mwenyekiti wa
Kamati ya Usajili ya Simba, Zacharia Hans Poppe, Mkude alisaini mkataba
huo mbele ya waandishi wa habari. Awali kulikuwa na taarifa kwamba Mkude
ameishaongeza mkataba Simba.
No comments: