Tuesday, July 8, 2014

MTOTO MIAKA 3 AJISAIDIA HAJA KUBWA KWA NJIA YA MDOMO

MASKINI Mungu wangu! Ndiyo maneno aliyoanza nayo kusema mama mzazi wa mtoto Salome Abdallah Said (3), kutokana na mwanaye huyo afya yake kuzidi kubadilika kufuatia kuumwa mara kwa mara licha ya kufanyiwa upasuaji mara mbili.
Mtoto Salome Abdallah Said (3) akiwa na kovu tumboni baada ya upasuaji.
Akizungumza na gazeti hili wiki iliyopita mama wa mtoto huyo Veronica Laurent, mkazi wa Bunju B, jijini Dar es Salaam alisema kwamba mwanaye kwa sasa hali yake siyo nzuri kwa vile amekuwa akijisaidia haja kubwa kupitia mdomoni kama hapo awali, hali hiyo anasema ameambiwa na madaktari inasababishwa na utumbo wake wa haja kubwa kujikunja.
Muonekano wa karibu wa kovu la Salome Abdallah Said.
HISTORIA YA MTOTO
Veronica anaeleza: “Mwanangu kwa sasa ana miaka mitatu, tangu nimzae katika Hospitali ya Mwananyamala, Dar, aligundulika ana matatizo ya kutojisaidia haja kubwa kama kawaida ilibidi nipelekwe Hospitali ya Muhimbili kwa uchunguzi zaidi.
“Nilimfikisha Muhimbili akiwa katika hali mbaya akawa anajisaidia haja kubwa kupitia mdomoni, hata hivyo, nikaambiwa tumpeleke Hospitali ya Agha Khan kwa vipimo zaidi, huko akagundulika kuwa utumbo wa haja kubwa umejikunja.”
Mtoto Salome Abdallah Said akiwa na mama yake.
AFANYIWA UPASUAJI MUHIMBILI
Katika maelezo yake mama huyo alisema kwamba mtoto wake alifanyiwa upasuaji kwa mara ya kwanza tumboni na kuwekwa tundu ambalo alikuwa akilitumia kutolea haja kubwa, baadaye akafanyiwa tena upasuaji kwa mara ya pili chini ya tumbo na kuwekewa utumbo bandia lakini hata hivyo, ulikuwa mwembamba hivyo ukawa haufanyi kazi vizuri.
UTUMBO WA BANDIA
“Tulipotoka Muhimbili na kurejea nyumbani haikuchukua siku nyingi hali ya mtoto ikazidi kuwa mbaya, akawa analia kila mara nikaamua kurudi Muhimbili.
“Madaktari baada ya uchunguzi wakasema utumbo wa bandia aliowekewa ulikuwa mdogo na mwembamba hivyo ulishindwa kufanya kazi pia utumbo ulikuwa umejikunja.
“Niliambiwa zinahitajika shilingi laki tisa ili afanyiwe matibabu ambapo nimeshindwa kuzipata, bora awamu ya kwanza alijitokeza mdhamini akatoa shilingi laki tisa. Nawaaomba Watanzania wenzangu wamsaidie mwanangu ili kumnusuru na kifo, maana madaktari wamesema bila kufanyiwa hivyo anaweza kupoteza maisha,” alisema mama huyo.
Akifafanua zaidi alisema: “Wakati fulani ili apitishe haja kubwa katika njia ya kawaida inabidi ninunue dawa ya kulainisha kinyesi kwani bila kufanya hivyo ni lazima ajisaidie kwa kupitia mdomoni.”
BABA YAKE ATOROKA
“Kwa sasa mtoto halali kutokana na kulia kutokana na maumivu makali, baba yake baada ya kuona tatizo la huyu mwanangu alitoweka na kuzima simu, hapatikani. Mimi nashindwa kufanya kazi yoyote.
Nawaomba Watanzania mnisaidie kupitia namba yangu ya simu 0712 004 677 au 0767 026 551,” alisema mama huyo huku akilengwalengwa na machozi.

No comments:

Speak Your Mind

Powered By Blogger · Designed By Seo Blogger Templates