Friday, July 11, 2014

ANAOMBA MSAADA WAKO ASIENDELEE KUOZA MGUU

kijana Peter  Sitiwati akiwa na maumivu makali yaliyosababishwa na kuoza kwa mguu.
 AMA kweli ng’ombe wa maskini hazai, kijana Peter  Sitiwati (26), mkazi wa Sinza ya kwa Remmy jijini Dar amejikuta akikatisha ndoto za utafutaji maisha kufuatia kuoza mguu baada ya ajali mbaya ya gari.Akizungumza na mwandishi wetu jijini Dar juzi kati kwa sauti ya kukata tamaa, Peter alisema alipata ajali ya gari mwaka 2013 maeneo ya Sinza-Mori, Dar na kuumia vibaya mguu wa kulia.’’Baada ya kugongwa na gari niliangukia mtaroni nikachomwa na kijiti kwenye mguu wa kulia. Nilikimbizwa Hospitali ya Palestina kutibiwa na baada ya muda mguu ulionesha kupona kwa juu, lakini kumbe ndani kidonda kilikuwa kibichi na kiliendelea kulika bila mimi kujua.
 “Mwanzoni mwa mwaka huu (2014) nikaanza kushangaa usaha mwingi unatoka sehemu mbalimbali ya mguu tena na harufu mbaya, mguu ukaonekana umeoza tena una matundu matatu, si unauona ulivyo, hata watu hawapendi kukaa jirani na mimi,” alisema Peter huku akionesha mguu wake huo.



Muonekano wa mguu wa Peter  Sitiwati.

 Peter alisema atashukuru kama atapata nauli ya kurudi kwao, Makambako, Njombe kwa vile ameona maisha magumu huku akiishi kwa kushindwa kula na kulala kwa shida.
 “Ila namshukuru sana msamaria mwema anaitwa Louis, ndiye anayenisaidia kwa sasa,” alisema.

Aliongeza kuwa, baada ya kuhangaika kusaka nauli bila mafanikio, baadhi ya watu walimwambia atoe taarifa kwenye Magazeti Pendwa ya Global Publishers ambayo yanasomwa na watu wengi Tanzania, atasaidiwa.
 “Napenda kuwaomba Watanzania mnaosoma Magazeti Pendwa ya Shigongo mnichangie pesa ili nipate matibabu na nauli ya kurudi  kwetu. Wenye kuguguswa na tatizo langu wanaweza kunisaidia kwa kutumia namba ya simu 0716 122 780,  Louis.

No comments:

Speak Your Mind

Powered By Blogger · Designed By Seo Blogger Templates