Wednesday, May 28, 2014

TETESI ZA SOKA KWENYE MAGAZETI YA UINGEREZA NA TOVUTI ZA ULAYA

Boss mpya wa Tottenham Mauricio Pochettino anataka kumchukua nahodha wake wa zamani Adam Lallana (Guardian), Chelsea bado wanamnyatia Rafael Varane kutoka Real Madrid kuziba pengo la David Luiz (Daily Star), Edin Hazard amefutilia mbali taarifa kuwa anataka kwenda PSG (London Evening Standard), Man United wanamfuatilia kiungo wa PSG Adrien Rabiot, ambaye pia ananyatiwa na Arsenal, Chelsea na Man City (Daily Mail), Harry Radknapp Wa QPR amekiri kuwa itakuwa ngumu kutomzuia Loic Remy kuondoka- Liverpool, Arsenal na Chelsea wameonesha nia ya kumtaka (Daily Express), Chelsea wamekubali kumsaini tena Tiago kutoka Atlètico Madrid (Daily Mail), Arsene Wenger huenda akamchukua tena Kim Kallstrom kwa mkopo (Daily Mirror), Niklas Bendtner anasakwa na timu nne baada ya kutoswa na Arsenal- Leicester City, Burnley, Crystal Palace na Hull City (Sun), Monaco wanamtaka Alexander Kolarov Wa Man City (Sun), Chelsea wapo tayari kulipa paundi milioni 19.4 kumchukua beki wa kushoto wa Atlètico Madrid Filipe Luis (Marca).
NA HATIMAYE.. Kitabu kipya kilichotoka kinasema striker wa Real Madrid na Ureno, Cristiano Ronaldo ana mfupa wa ziada kwenye mkuu wake wa kulia unaomsaidia katika kupiga free kick au zuruba, limeandika The Sun. Share tetesi hizi na wapenda soka wote. Tetesi nyingine kesho tukijaaliwa


chanzo Salim Kikeke

No comments:

Speak Your Mind

Powered By Blogger · Designed By Seo Blogger Templates