Tuesday, May 6, 2014

Sare ya 3-3 yamliza Luis Suarez

Luis Suarez alia baada ya Liverpool kwenda sare ya mabao matatu na Crystal Palace
Liverpool wameona giza huku kombe la Ligi ya Premier likiwakwepa baada ya kwenda sare ya mabao matatu dhidi ya Crysral Palace .
Cha kushangaza ni kwamba Liverpool walikuwa mbele kwa mabao matatu lakini Cyrstal walitifua kivumbi na kutoka nyuma bila bao huku wakimaliza mechi kwa mabao matatu sawa na Liverpool.
Joe Allen, Daniel Sturridge na Luis Suarez waliiweka mbele klabu yao katika muda wa saa moja kwa mabao matatu.
Lakini Damien Delaney na Dwight Gayle walipunguza pengo hilo na kuingiza mabao matatu katika muda wa dakika mbili katika kipindi cha pili cha mechi.
Hali hii iliwachaa mashabiki wa Liverpool vinywa wazi wasijuie cha kusema.
Liverpool sasa wako mbele ya Man City kwa poiti moja tu kwenye jedwali la alama.City bado wako na mechi moja kucheza.
City watamenyana na Aston Villa katika uwanja wa Etihad mnamo siku ya Jumatano, kabla ya kumaliza msimu kwa mechi nyingine dhidi ya West Ham Jumapili.

No comments:

Speak Your Mind

Powered By Blogger · Designed By Seo Blogger Templates