Sunday, March 16, 2014

RIDHIWANI KIKWETE AANZA KAZI YA KUZISAKA KURA JIMBO LA CHALINZE

Mgombea Ubunge katika Uchaguzi Mdogo wa Jimbo la Chalinze,Ridhiwani Jakaya Kikwete akitoa hotuba yake kwa wakazi wa Kijiji cha Miono,Wilayani Bagamoyo leo Machi 15,2014,ikiwa ni sehemu ya muendelezo wa Mikutano ya Kampeni zake za Uchaguzi huo mdogo wa Jimbo la Chalinze unaotarajiwa kufanyika Aprili 6,2014.Picha zote na Othman Michuzi.
Mgombea Ubunge katika Uchaguzi Mdogo wa Jimbo la Chalinze,Ridhiwani Jakaya Kikwete pamoja na Meneja wa Kampeni za Uchaguzi Mdogo wa Jimbo la Chalinze,Steven Kazidi wakiwa na Mama wa Mbunge wa Zamani wa Jimbo la Chalinze (aliefariki Dunia),Marehemu Said Bwanamdogo wakati walipofika kumjulia hali nyumbani kwake Kijijini Miono,Bagamoyo leo Machi 15,2014.
Meneja wa Kampeni katika Uchaguzi Mdogo wa Jimbo la Chalinze (CCM),Steven Kazidi akisisitiza jambo wakati wa Mkutano wa Kumpigia debe Mgombea Ubunge katika Jimbo hilo,Ridhiwani Jakaya Kikwete (hayupo pichani),uliofanyika leo Machi 15,2014 kwenye Kijiji cha Kimange.
"Kinamama huko,inamaana hakuna vigelegeleeeee .....???" hivyo ndivyo alivyokuwa akiuliza Diwani wa Kata ya Kimange,Hussein Hading'oka (pichani) wakati alipokuwa akimwaga sifa kede kede kwa Mgombea Ubunge wa Jimbo la Chalinze,Ridhiwani Jakaya Kikwete.
Mgombea Ubunge katika Uchaguzi Mdogo wa Jimbo la Chalinze,Ridhiwani Jakaya Kikwete akiwapungia mkono wananchi wa Kijiji cha Kimange,Kata ya Kimange,Wilayani Bagamoyo leo Machi 15,2014, wakati akiwasili kwa ajili ya Mkutano wa Kampeni zake za Uchaguzi huo mdogo unaotarajiwa kufanyika Aprili 6,2014.Picha zote na Othman Michuzi.
Meneja wa Kampeni katika Uchaguzi Mdogo wa Jimbo la Chalinze (CCM),Steven Kazidi (kulia) akizungumza jambo na Mgombea Ubunge wa Jimbo la Chalinze,Ridhiwani Jakaya Kikwete kabla ya kumpatia kipaza sauti ili aweze kuzungumza na wanakijiji wa Kimange.

BOFYA READ MORE KWA PICHA ZAIDI

Mgombea Ubunge katika Uchaguzi Mdogo wa Jimbo la Chalinze,Ridhiwani Jakaya Kikwete akiwahutubia wananchi wa Kijiji cha Kimange,Kata ya Kimange Wilayani Bagamoyo leo Machi 15,2014,wakati wa Mkutano wa Kampeni zake za Uchaguzi huo mdogo wa Jimbo hilo unaotarajiwa kufanyika Aprili 6,2014.
Mgombea Ubunge katika Uchaguzi Mdogo wa Jimbo la Chalinze,Ridhiwani Jakaya Kikwete akijumuika pamoja na wanakijiji wa Miono,Wilayani Bagamoyo kwenye dua maalum ya kumuomba Mwenyezi Mungu ajaalie mafanikio mema katika kumuongoza Mgombea Ubunge huyo kwenye mwendelezo wa Kampeni zake.
Dua ikiendelea.......
wakiwa wamesimama kwa dakika moja kumkumbuka aliekuwa Mbunge wa Jimbo la Chalinze,Marehemu Said Bwanamdogo.
"Shkamoo Bibi....."
Ridhiwani akiendelea kumwaga sera zake.

Wananchi wakifatilia Hotuba ya Mgombea wao kwa Umakini mkubwa.
Wadau wa Kijiji cha Kimange wakichukua taswira ya Mgombea wao kupitia simu zao za mikononi.
"Mtoto Mzuri naomba Kofiaaaaa"
Wananchi wakimsikiliza Mgombea wako kwa makini.
Nyundo na Jembe ndio mpango mzimaaaa......
"Kijana wetu wewe ndie tunaekutaka,na amini utashinda kwa kishindo" ndivyo alivyosikika mama huyu akimwambia Mgombea Ubunge Jimbo la Chalinze,Ridhiwani Jakaya Kikwete.
Mkutano kwa siku ya leo ulimalizikia katika Kijiji cha Mbwewe,Pichani ni Mgombea Ubunge Jimbo la Chalinze akipita katikati ya vijana wa chipukizi wakati akiwasili kwenye Kijiji hicho.
Mgombea Ubunge Jimbo la Chalinze,Ridhiwani Jakaya Kikwete (kulia) akifurahia baada ya kupewa maneno ya kuvutia kutoka kwa vijana wa chipukizi.


No comments:

Speak Your Mind

Powered By Blogger · Designed By Seo Blogger Templates